Pia kulikuwa na watu waaminifu miongoni mwa Wayahudi

 

Leo inafanana sana na nyakati za awali, wakati pia kulikuwa na watu wengi ambao hawakutaka kujua kuhusu Mungu.

Wao ni watu waasi, . . . wasiotaka kusikia sheria ya Yehova.—Isa. 30:9.

Kwa kuwa watu walikataa kusikiliza, Isaya alitabiri kwamba Yehova angeruhusu wapatwe na msiba. (Isa. 30:​5, 17; Yer. 25:​8-11)

 Wote wataaibishwa Na watu ambao hawawezi kuwanufaisha, Ambao hawawapi msaada wowote wala manufaa yoyote, Isipokuwa aibu na fedheha.”+ (Isaya 30:5)

17 Watu elfu moja watatetemeka wakitishwa na mtu mmoja;+ Mtakapotishwa na watu watano mtakimbia Mpaka mbaki kama mlingoti juu ya mlima, Kama nguzo ya ishara juu ya kilima. (Isaya 30:17)

“Kwa hiyo Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘“Kwa sababu hamkuyatii maneno yangu, ninaziita familia zote za kaskazini,”+ asema Yehova, “ninamwita Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni, mtumishi wangu,+ nami nitawaleta dhidi ya nchi hii+ na dhidi ya wakaaji wake na dhidi ya mataifa haya yote yanayozunguka.+ Nitawaangamiza na kuwafanya kuwa kitu cha kutisha na kitu cha kupigiwa mluzi na magofu ya kudumu. 10 Nitakomesha sauti ya furaha na sauti ya shangwe ndani yao,+ sauti ya bwana harusi na sauti ya bibi harusi,+ sauti ya jiwe la kusagia na nuru ya taa. 11 Na nchi hii yote itakuwa magofu na kitu cha kutisha, na mataifa haya yatalazimika kumtumikia mfalme wa Babiloni kwa miaka 70.”’+

12 “‘Lakini miaka 70 itakapotimia,+ nitamfanya mfalme wa Babiloni awajibike* na pia taifa hilo kwa sababu ya kosa lao,’+ asema Yehova, ‘nami nitaifanya nchi ya Wakaldayo kuwa mahame na ukiwa daima.+ 13 Nitatimiza maneno yangu yote niliyosema dhidi ya nchi hiyo, yote yaliyoandikwa katika kitabu hiki ambayo Yeremia ametabiri dhidi ya mataifa yote. 14 Kwa maana mataifa mengi na wafalme wakuu+ watawafanya kuwa watumwa,+ nami nitawalipa kulingana na matendo yao na kazi ya mikono yao wenyewe.’”+ (Yeremia 25:8-11-14)

Na kwa kweli, Wababiloni waliwapeleka utekwani. Hata hivyo, kulikuwa na baadhi ya watu waaminifu miongoni mwa Wayahudi, na Isaya aliwaambia kwamba siku moja Yehova angewaonyesha tena kibali chake. (Isa. 30:​18, 19)

18 Lakini Yehova anangoja kwa subira* ili kuwaonyesha kibali,+ Naye atainuka ili kuwaonyesha rehema.Kwa maana Yehova ni Mungu wa haki.+ Wenye furaha ni wote wanaoendelea kumtarajia.*+

19 Watu watakapokaa Sayuni, Yerusalemu,+ hamtalia kamwe.+ Kwa hakika atawaonyesha kibali mara tu atakaposikia kilio chenu cha kuomba msaada; atawajibu mara tu atakaposikia kilio chenu.+ 20  (Isaya 30:18-19)

Na hivyo ndivyo ilivyotokea. Yehova aliwaweka huru kutoka utekwani Babiloni. Hata hivyo, hawakukombolewa papo hapo. Maneno

“Yehova anangoja kwa subira ili kuwaonyesha kibali,”

yalionyesha kwamba muda fulani ungepita kabla ya watu wake waaminifu kukombolewa. Kwa kweli, Waisraeli walikaa miaka 70 uhamishoni huko Babiloni kabla ya baadhi yao kuruhusiwa kurudi Yerusalemu. (Isa. 10:21; Yer. 29:10)

21 Ni watu wachache tu waliobaki watakaorudi, Watu wa Yakobo waliobaki, watarudi kwa Mungu Mwenye Nguvu.22 Kwa maana ingawa watu wako, ewe Israeli,Ni kama chembe za mchanga wa bahari,Ni watu wachache tu waliobaki watakaorudi.Maangamizi yameamuliwa,Na haki* itawafunika.+

23 Naam, maangamizi yaliyoamuliwa na Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi, Yatatekelezwa katika nchi yote.+ (Isaya 10:21-23)

10 “Kwa maana Yehova anasema hivi: ‘Miaka 70 itakapotimia huko Babiloni nitawakazia ninyi fikira,+ nami nitatimiza ahadi yangu kwa kuwarudisha mahali hapa.’+

11 “‘Kwa maana ninajua vizuri mawazo ninayofikiria kuwaelekea ninyi,’ asema Yehova, ‘mawazo ya amani, wala si ya msiba,+ ili niwape ninyi wakati ujao na tumaini.+ 12 Nanyi mtaniita na kuja na kusali kwangu, nami nitawasikiliza.’+

13 “‘Mtanitafuta na kunipata,+ kwa maana mtanitafuta kwa moyo wenu wote.+ 14 Nami nitawaruhusu mnipate,’+ asema Yehova. ‘Nami nitawakusanya mateka wenu na kuwakusanya ninyi pamoja kutoka katika mataifa yote na sehemu zote nilizowatawanya,’+ asema Yehova. ‘Nami nitawarudisha mahali nilipowatoa nikawapeleka uhamishoni.’+ (Yeremia 29:10-14)

Watu hao waliporudi katika nchi yao, machozi ya huzuni yalibadilika na kuwa machozi ya shangwe.