Kukua kwa upendo na kufanya maendeleo

 

Kupitia upendo na tuendelee kukua katika mambo yote.—Efe. 4:15.

Baada ya kubatizwa, sisi sote tunahitaji kufuata ushauri ambao mtume Paulo aliwapa Wakristo wenzake huko Efeso. Aliwatia moyo wawe Wakristo ‘waliokomaa kabisa.’ (Efe. 4:13)

Kwa maneno mengine, ni kama aliwaambia hivi:

‘Endeleeni kufanya maendeleo.’

Tayari unampenda Yehova sana. Lakini upendo wako kwake unaweza kuongezeka hata zaidi. Jinsi gani? Mtume Paulo alitaja njia moja kwenye andiko la Wafilipi 1:9.

Na hili ndilo ninaloendelea kusali, kwamba upendo wenu uwe mwingi zaidi na zaidi+ pamoja na ujuzi sahihi+ na utambuzi kamili;+

Paulo alisali kwamba upendo wa Wafilipi uwe

“mwingi zaidi na zaidi.”

Basi, upendo wetu kwa Yehova unaweza kuongezeka. Tunaweza kufanya hivyo kwa kujipatia

“ujuzi sahihi na utambuzi kamili.”

Kadiri tunavyozidi kumjua Yehova, ndivyo tunavyozidi kumpenda na kuthamini sifa zake na njia yake ya kufanya mambo. Tamaa yetu ya kumfurahisha inaongezeka, na tunajitahidi kuepuka kufanya jambo lolote ambalo halitampendeza. Tunajitahidi kutambua mapenzi yake na jinsi tunavyoweza kumtii. w22.08 2-3 ¶3-4