Maandiko ya Biblia kuhusu mtazamo wa kuja pamoja

Te herinneren - Kukumbuka - Se souvenir - to Remember

 

Quotes from God’s Word.

“Tusiache ile desturi ya kukutana pamoja, kama vile wengine wanavyofanya. Bali tunapaswa kusaidiana kwani, kama mwonavyo, Siku ile ya Bwana inakaribia.” (Hebrews 10:25 Swahili)

“Kwa maana popote pale wanapokusanyika wawili au watatu kwa jina langu, mimi nipo hapo kati yao. »” (Matthew 18:20 Swahili)

“Hawa wote waliendelea kujifunza kutoka kwa mitume, kuishi pamoja kidugu, kumega mkate na kusali.” (Acts 2:42 Swahili)

Huwaongoza wanyenyekevu katika haki,
naye huwafundisha njia yake.
” (Psalms 25:9 Swahili)

Ingawa Bwana yuko juu,
humwangalia mnyonge,
bali mwenye kiburi
yeye anamjua kutokea mbali.
” (Psalms 138:6 Swahili)

Mtu mwenye haki na anipige: ni jambo la huruma;
na anikemee: ni mafuta kichwani mwangu.
Kichwa changu hakitalikataa.

Hata hivyo, maombi yangu daima
ni kinyume cha watenda mabaya,
” (Psalms 141:5 Swahili)

“Mimi ndiye mwenye kumwonya na kumrudi yeyote ninayempenda. Kwa hiyo kaza moyo, achana na dhambi zako.” (Revelation 3:19 Swahili)

“Nimekuwa nikiwapeni daima mfano kwamba kwa kufanya kazi mithili hiyo tunapaswa kuwasaidia walio dhaifu, tukikumbuka maneno ya Bwana Yesu mwenyewe: <Heri zaidi kutoa kuliko kupokea. »>” (Acts 20:35 Swahili)

Yeye amhurumiaye maskini humkopesha Bwana,
naye atamtuza kwa aliyotenda.
” (Proverbs 19:17 Swahili)

“Wapeni wengine wanavyohitaji, nanyi mtapewa. Naam, mtapokea mikononi mwenu kipimo kilichojaa, kikashindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika. Kwa maana kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho ambacho Mungu atatumia kwenu. »” (Luke 6:38 Swahili)

“Lakini kila mmoja na aupime vizuri mwenendo wake mwenyewe. Ukiwa mwema, basi, anaweza kuona fahari juu ya alichofanya bila kuwa na sababu ya kujilinganisha na mtu mwingine.” (Galatians 6:4 Swahili)

 

+

Uliopita

  1. Upendo ulioonyeshwa
  2. Mahali pa kukutania ili kushiriki amani na upendo wao kwa wao
  3. Matunda ya wenye haki na wapenda amani
  4. Nyumba yenye udongo wenye rutuba iliyojaa mimea ya upendo
  5. Fanya mpango wa kupata marafiki
  6. Bwana Mungu hutufanya tukutane na kukua
  7. Jumuiya ya imani kuchukua mwenge
  8. Kuja pamoja ili kutoa bora zaidi kwa wengine